Yapo mazoezi ya aina mbalimbali yanayo kusaidia katika kujenga mwili hususani kwa mwanaume
01.Pushup
Hili ni zoezi zuri sana katika kujenga mwili, kufanya zoezi hili hufanya kutanua kifua hivyo unakua na pumzi ya kutosha ndo maana wakimbiaji wengi wa mbio fupi kama vile mita mia zoezi kubwa kwao wanalokua wanalifanya ni kupiga pushup
pia pushup inasaidia kujaza misuli ya mikono hivyo kwa wale wanao fanya kazi ya kupigana linakua zoezi hili ni muhimu sana kwao
pia pushup inakufanya mwili wako kua na balance hivyo hata ukiwa unakimbia kwa spidi kali sana hautaweza kudondoka kirahisi.
02.Kunyanyua vitu vizito(gmy).
Zoezi la gym ni sawa kabisa na na pushup kwani linasaidia kujenga misuli ya mikono na na kutanua kifua
umhimu wa mazoezi haya
1. MAZOEZI YA KUNYANYUA VITU VIZITO YANAONGEZA UWEZO WA AKILI KUFANYA KAZI VIZURI Mazoezi ya kunyanyua vyuma yanachochea uzalishaji wa homoni kama BDNF (Brain-Derived Neurotrophic Factor), homoni hizi husaidia uzalishaji wa seli mpya za ubongo. Bila kusahau mazoezi ya kunyanyua vitu vizito yanachangia kwa kiasi kikubwa kuongeza ukubwa wa ” hippocampus”,hii ni sehemu ya ubongo inayohusika na uhifadhi kumbukumbu. Unataka kuwa “smart” kwa kichwa?
Kama jibu ni ndiyo, basi anza kufanya mazoezi ya kunyanyua vitu vizito, lakini usiache kusoma vitabu pia.
2. MAZOEZI YA KUNYANYUA VITU VIZITO YANAONGEZA FURAHA Watu wanaonyanyua vitu vizito ni watu wenye furaha sana. Ni kawaida kumuona mtu anayefanya mazoezi ya kunyanyua vitu vizito akiwa na tabasamu muda wote. Hali hii inasababishwa na uzalishaji mkubwa wa kemikali za “endorphins” kwenye miili ya watu wanaonyanyua vitu vizito. Kemikali hizi huzalishwa mwilini kwa lengo la kuufanya mwili usihisi maumivu pindi unapofanya mazoezi ya Kunyanyua vitu vizito. 3. MAZOEZI YA KUNYANYUA VITU VIZITO YANALETA ULALAJI MZURI Watu wanaonyanyua vitu vizito huwa wanalala usingizi mzuri sana, huwa hawana matatizo ya kukosa usingizi. Ulalaji mzuri ni sehemu ya kujenga afya, anza kufanya mazoezi haya. 4. MAZOEZI YA KUNYANYUA VITU VIZITO YANAONGEZA HOMONI ZA KIUME Watu wanaonyanyua vitu vizito wana kiwango kikubwa sana cha homoni za testosterone, hizi ni homoni muhimu katika kujenga mwili wa mwanaume. Kiwango kidogo cha homoni za testosterone huweza kusababisha uchovu, kudumaa na kukosa nguvu za kiume.
5. MAZOEZI YA KUNYANYUA VITU VIZITO YANAONGEZA UWEZO WA KUJIAMINI Watu wanaonyanyua vitu vizito ni watu wanaojiamini sana, hii inasababishwa na miili yao kujengeka vizuri. Lakini pia utafiti unaonesha kuwa kitendo cha kunyanyua vitu vizito pekee kinatosha kukufanya ufurahie muonekano wa mwili wako hivyo hiyo hali inakuongezea uwezo wa kujiamini mbele za watu.
Asante endelea kufuatilia kurasa zetu na subscribe Channel Yetu Ya Youtube tiztu kwa habari na video zote zinazohusu Afya ,chakula na mazoezi.
https://youtu.be/RcxdLwC-reg Kalori ni nini? Kwa ufupi, kalori ni kitengo kinachopima nishati. Kalori hutumiwa kupima maudhui ya nishati ya vyakula na...
https://www.youtube.com/watch?v=iE8k-i0X9Xk&t=1s Jinsi Ya Kufanya Mazoezi Ya Body Balance Mazoezi ya Body balance yanasaidia sana katika msawaziko wa mwili na katika...
https://www.youtube.com/watch?v=qQiuay9fzAQ&t=1s Aina (4) Za Mazoezi Ya Kuzuia Maumivu Ya Hedhi Maumivu ya hedhi ni tatizo kubwa kwa wanawake wengi, hivyo...
https://www.youtube.com/watch?v=66VqjncGw0o Jinsi Ya Kufanya Zoezi La Squat Japo kuwa Squat ni zoezi zuri sana, lakini ukilikosea linaweza kukupa madhara badala...
https://www.youtube.com/watch?v=BoHY7B4M_EE Jinsi Ya Kutumia Tairi Katika Kujenga Mwili Wako Tairi ni moja ya nyenzo muhimu sana itakayo kusaidia katika mazoezi...
https://www.youtube.com/watch?v=QDu-HMqozgA&t=1s Kubadilisha lishe kunaweza kupunguza kwa kiasi kikubwa shinikizo la damu. Utafiti umeonyesha kuwa vyakula fulani vinaweza kupunguza shinikizo la...