
Je, Ni vitu gani vinasababisha uzito kubadilika mara kwa mara?
Ni kitu cha kushangaza lakini ndo ukweli, mara nyingi kama umeshwahi kupima uzito na kuanza mchakato wa kupunguza uzito unaweza kushangwazwa na jinsi uzito wako unayobadilika badilika kama kinyonga, yaani leo unaweza kuwa na Kg 68 kesho 69 keshokutwa 65. Unazani hii husabishwa na nini?
Wakati mwingine sababu ya mabadiliko ya uzani wa kila siku ni dhahiri.Labda unakula chakula kingi kabla ya kulala wakati ambao ulisababisha kupata uzito, au umefanya mazoezi makali yaliyo sababisha kupunguza uzito.
Ikiwa unajaribu kupunguza uzito au kujenga mwili wako, unaweza kushawishika kuamini kwamba mabadiliko ya kila siku ya uzito wako yanasababiswa na kuchoma mafuta au kuongezeka mafuta mwilini. Inawezekana ikawa kweli lakini kuna mambo mengine mengi yanayoathiri uzito wako .
Wataalamu wa Afya wanasema kwamba uzito wako kubadilika kwa kupungua au kuongezeka kilo 2.5(kg) kwa siku ni kitu cha kawaida kwa watu, na unaweza kubadilika hadi 10kg kwa siku kwa watu wenye uzito au miili mikubwa.
Sababu za uzito wako kuwa na madabiliko ya mara kwa mara kila siku zinaweza kuwa kama zifuatazo.
Mabadiliko ya uzito kutokana na chunvi

Madini ya sodiamu ambyao hupatikana kwenye mwili husabisha mwili kufyonza maji na na kuyahifadhi mwilini, hali hii itasabisha uzito wa mwili unaotokana na maji kuongezeka. Na hii hutofauriana kuendana na mtu, kuna wengine miili yao hufyanza maji sana kutoka kwenye chumvi na mingine haifanyi hivyo.
Vilevile vyakula vya Baridi, vyakula viliyogandishwa na vyakula vyenye ladha tamu mara nyingi vinakua na kiasi kingi cha sodiamu.
Kama umeshawahi kunywa supu au mtoli wenye chumvi nyingi unaweza kushangaa kuongezeka kilo kadhaa ndani ya masaa machache.
Ni vema kuzingatia ulaji bora wa chumvi na vyakula vyenye sodiam kwa wingi ili kuweza kupunguza uzito kirahisi.
Uzito Kubadilika kutokana na matumizi ya wanga

Kama ni mpenzi wa Ugali, mikate, tambi, mchele na wanga nyinginezo, basi fahamu kwamba uzani wako unaoongezeka kwa siku kwa haraka unasabiswa na matumizi makubwa ya chakula cha wanga unachokula.
Wataalamu wa afya wanasema kwamba kwa kila gramu 1 (1g) ya wangu unayoingiza mwilini mwako, mwili wako utabaki takriban na gramu tatu za maji kwenye mwili wako ili kuweza kutunza nishati inatotokana na wanga.
Kwa sababu hiyo ikiwa unakula sana vyakula vya wanga , uzito wako utaongezeka sio kwa sababu ya mafuta yameongezeka bali kwa sababu uzito wa maji umeongezeka kwenye mwili wako. Na kama ulika vyakula vyenye wanga na chumvi nyingi kama vile wali wenye chumvi nyingi kwa pamoja basi uzito utaongezeka mara dufu.
Uzito Kubadilika kutokana na kiasi cha chakula unachokula.

Chakula tunachokula huwa kinaongeza uzito kwenye miili yetu pia. Mara nyingi vyakula hivi huwa vina maji maji na uzito mwingine ambao unapokula huongeza uzani wetu Hata baada ya chakula kusagwa na kusabazwa mwilini bado uzani wa taka mwili kama kinyesi na mkojo huuongeza pia uzito kwenye mwili wako
Kulingana na wataalam, utumiaji wa vikombe viwili vya maji huongeza uzito wako kwa 0.5kg.
Kiasi cha chakula unachokula kinasababisha uzito wako upongezeke au upungue kama u,
Uzito Kubadilika kutokana kinyesi kwenye utumbo mpana.

Najua wengi hampendi kuzungumzia vinyesi venu……! Ila hili ni soma lazima tujifunze, hivi unafahamu kwamba kinyesi kina uzito? unajua kilogramu ngapi za kinyesi unachotoa kwa siku? Unatafiti watafiti, wachunguzi wamegundua kwamba unaweza kutoa gramu 125 hadi 170 za kinyesi kwa siku, na hii na kwa wale wanaoenda haja kubwa mara moja kwa siku.
Hata hivyo, tafiti zingine zinaripoti wastani wa uzani wa kinyesi kwa siku takribani gramu 106.
Hata baada ya kuondoa kinyesi mwilini mwetu bado taka mwili kama vile mikojo na Mzunguko mrefu wa chakula kwenye utumbo unasabaisha chakula hicho kifyonzwe zaidi hivyo hutaona mabadiliko makubwa kwenye uzito wa mwili wako
Uzito Kubadilika kutokana Ufanyaji mazoezi.

Kufanya mazoezi kunaweza kupunguza uzito wa maji mwilini kutokana na kutokwa jasho jingi sana. Wataalamu wanasema kwamba kwa kawaida mtu hupoteza Lita 0.7 hadi 1.4 kwa kufanya mazoezi ndani ya lisaa limoja, japokuwa kiwango hiki hutegemea na hali ya hewa na mwili wa mtu inaweza kuwa juu au chini ya hapo. Hivyo kutokwa jasho kunaweza kupunguza kilo zako.
Ukiona kuwa umepunguza uzito mara kwa mara baada ya mazoezi, utahitaji kuja pamoja na mpango ulioboreshwa wa kuongeza maji mwilini.
Aina nyinginezo za mazoezi zinaweza kusababisha mabadiliko ya uzito wako kwa kuoungeza, sishangae……. mazoezi yanaweza kuongeza uzito wako pia. Mazoezi kama ya Kuinua vitu vizito na ya kukuza misuli kama vile push up, squat husabisasha uzito wa mwili kuongezeka. Kwa sababa mazoezi haya husabaisha mikwaluzo kidogo kwenye misuli hivyo misuli hufyonza maji ili kutengeneza misuli hii husabisha misulu kutanuka na kukua, mazoezi haya hutumiwa zaidi na wanaotaka kushape mwili na kujenga mwili.
Uzito Kubadilika kutokana matumizi ya dawa

Kuna daadhi ya madawa huathiri jinsi mwili wako unavyofanya kazi, huongeza au kupunguza hamu ya kula na huweza kuathiri mmeng’enyo wa chakula mwilini mwako, hali hii husabisha uzito wa mwili wako kupungua au kuongezeka kuendana na dawa husika.
Iwapo una tumia dawa ya kutibu magonjwa kama vile kisukari, shinikizo la damu, matatizo ya mhemko, mshtuko wa moyo, maumivu wa kichwa, unaweza kugundua mabadiliko ya uzito katika mwili wako.
Usiache kutumia dawa endapo utaona mabadiliko ya uzito wako mwilini, na badala yake zungumza na daktari wako au mfamasia. Wakati mwingine uzito unakuwa wa kawaida unaotarajiwa, lakini wakati mwingine unaweza kuashiria kuwa kuna kitu kibaya.
Uzito Kubadilika kutokana Hedhi kwa mwanamke.

Wanawake wengi watapata ungezeko la maji mara na kabla ya kipindi chao cha hedhi, ongezeko la maji haya hufikia kilele cha juu siku moja baada ya kuanza hedhi. Kiwango hiki hupungua baada ya hedhi na uongezeka karibia na kipindi cha uchevushaji(ovulation) wa mayai.
Watafiti wengine wamegundua kwamba uhifadhi wa maji hautokani tu na mabadiliko ya homoni za ovari. Bali pia husababiswa na mabadiko ya maswaziko wa mwili na akili ambao unaweza kukupelekea kula sana au kutokula
Iwapo unajaribu kupunguza uzito wakati wa kipindi chako cha hedhi, ni muhimu kufahamu na kudhibiti wa chakula chako.
Uzito Kubadilika kutokana utumiaji wa vileo.

Inawezekana unaweza kugundua mara moja uzito kupungua kutokana na matumizi ya vileo kuliko kawaida. Watafiti wamegundua hivi vileo vinaweza kutoa mkojo ndani ya dakika 20 na kuondoa kiwango kikubwa cha maji mwilini ndani ya mda mchache.
Hata hivyo, Kupunguzwa kwa maji mwilini kutokana na pombe huwa kunaufanya mwili kutafuta maji mengine kutoka kwenye chakula utakachokula. Hali hii itasababisha upungue uzito wakati ukiwa unakunywa na uongezeke uzito baade.
Lini uzito wangu utarudi kawaida?.

Mabadiliko haya ya uzito kwa siku sio jambo la kukuogopesha, Uzito huu hutokana na kuongezeka kwa maji na wala sio mafuta. Usiwe na wasiwasi mbadiliko haya yanapotokea cha kuzingatia ni kuendelea na mtindo bora wa maisha na chakula bora
Je, ni wakati gani unapaswa kuwa na wasiwasi kuhusu mabadiliko ya uzito wa kila siku?

Unaweza kuwa na wasiwasi kuhusu mabadiliko ya haraka ya uzito wako endapo uzito wako utaendelea kuongezea au kupungua ndani ya siku saba bila kubadilika. Mf leo umeongezeka kg 3 kesho zinaongezeka tena haraka , kesho kutwa hivyo hivyo au leo umepungua, kesho tena kilo zinapungua haraka ndani ya siku 5 au 7. Ukiona hali hii basi kunaweza kuwa na tatizo kwenye mwili wako wahi hospitali haraka!
TAZAMA VIDEO KUJIFUNZA ZAIDI
Asante endelea kufuatilia kurasa zetu na subscribe Channel Yetu Ya Youtube tiztu kwa habari na video zote zinazohusu Afya ,chakula na mazoezi.
