
Je, wanga ni nini na vina nafasi gani katika mwili?
Wanga ni sehemu muhimu ya chakula, na vyakula vingi vya wanga hutoa faida bora za afya.
Kumekuwa na mitazamo mibaya mingi sana inayo zungumziwa kuhusiana na vyakula vya wanga hususani katika zama hizi. Lakini wanga ni moja ya virutubisho vikuu ambavyo mwili unahitaji, pamoja na protini na mafuta. Wanga ni muhimu sio tu kwa ajili kuishi na kufanya kazi ipasavyo, bali pia kustawisha mwili.
Ingawa wanga zilizosafishwa huchakatwa(kukobolewa) kwa ujumla hupunguza thamani ya virutibisho, kuliko zile ambazo haijachakatwa. Vyanzo vyote vya chakula vya wanga kawaida ni lishe bora kwa afya.
Hapa Tutanaenda kuona vyakula bora 11 vya wanga na faida zake mwilini.
Vyakula vya wanga vinavyo tokana na mbogamboga
Hivi ni ujumuisho wa vyakula kama vile:
1. Viazi vitamu

Viazi vitamu hupendelewa sana kujumuishwa katika milo mbalimbali.
C.A Utafiti wa 2015 iligundua kuwa baadhi ya molekuli za kabohaidreti katika viazi vitamu vya zambarau zinaweza pia kuwa antioxidant na antitumor.
Kiazi kitamu kimoja cha kati, kilichookwa au kuchemswa na ngozi kina gramu 23.61 (g) ya wanga. Viazi vitamu pia ni chanzo kizuri cha madini potasiamu na vitamini A . pia kwenye kundi hili inajumuisha magimbi, mihogo na shelisheli
2. Beets

Beetroots, au beets, ni mboga ya mizizi tamu, zambarau ambayo watu wanaweza kula mbichi au kupikwa.
Kikombe kimoja cha beets mbichi kina 13 g ya wanga.
Beets pia inakiwango kingi cha madini potasiamu, kalsiamu, folate, na vitamini A.
Pia huwapa watu nitrati isokaboni ambayo inawezakusaidia katika afya ya moyo.
3. Mahindi

Mahindi yasiyo kobolewa kwa ujumla ni afya tosha.
Mahindi ni chakula maarufu ambacho watu wanaweza kutumia mwaka mzima toka yakiwa bado mabichi na kuayala kwa kuchemshwa kula kande au yakiwa yamechomwa hadi yanapo vunwa na kusagwa kuwa unga na kula kama ugali.
Kulingana na Utafiti wa 2007, unaonyesha kwamba mahindi yana manufaa kwa kudhibiti viwango vya sukari ya damu na shinikizo la damu.
5.Mtama na uwele

Dengu ambazo ni mbegu za mimea ya majani mapana, ni vyanzo vikubwa vya wanga. Aina za nafaka nzima hutoa protini na nyuzinyuzi na hutoa faida nyingi za kiafya.
4.Mchele wa kahawia

wali wakahawia na mweupe una kiwango kikubwa sana cha wanga. Kikombe kimoja cha wali wa kahawia kilichopikwa kina 36 g ya wanga. Nafaka hii pia ina kiwango kikubwa cha antioxidants.
5. Shayiri na ngano

Shayiri na ngano isiyokobolewa ni mojawapo ya vyakula chenye kiwango kikubwa sana cha wanga
Kikombe cha shayiri au ngano kinatoa gram 27 ya wanga, pamoja na 5g ya protini na 4g ya fiber.
Utafiti umeonyesha kuwa shayiri inaweza kuwa na faida kubwa sana kwa afya ya moyo na mishipa.
6. Ndizi mbichi

Ndizi moja ya wastani ina gram 26.95 ya wanga. Sawa na viazi vitamu, pia vina potasiamu na vitamini A na C nyingi. kutokana na kua na kiwango kikubwa cha potasiamu, ndizi ni nzuri kwa afya ya moyo na husaidia kupunguza shinikizo la damu
7. Maembe

Maembe ni mojawapo ya matunda yenye kiwango kikubwa cha wanga pia yana vitamini, potasiamu, na nyuzinyuzi. ,Kikombe kimoja cha maembe yaliyokatwakatwa kina gram 24 ya wanga Maembe pia yana vitamini A na C nyingi, potasiamu, na nyuzinyuzi.
8. Tende

Kuna aina nyingi za tende, na kwa asili ni tamu vya kutosha kutumika kama vitafunio vitamu Tende ina gram 17.99 ya wanga Tunda hili pia lina nyuzinyuzi nyingi, kalsiamu, fosforasi, potasiamu, na vitamini A.
9. Zabibu

Kikombe kimoja cha zabibu kina kiwango cha gram 129.48 ya wanga. Pia zabibu ina madini mengi sana kama vile potasiamu, magnesiamu, fosforasi, na kalsiamu.
Zabibu ni a chanzo kizuri cha antioxidants pia.
10. Maharage , njegere, mbaazi na kunde

Maharage ya mimea ya jamii ya mikunde ni chakula bora chenye wanga mzuri. Kikombe kimoja cha maharagwe kina gram 21 ya wanga. Pia ni chanzo kizuri cha protini na nyuzinyuzi.
Maharage haya pia yana madini potasiamu na chuma. Ulaji wa maharagwe meupe au meusi husaidia kuondoa uvimbe katika koloni.
11. Dengu

Dengu ni jamii ya kunde maarufu yenye protini nyingi.
Kikombe kimoja cha dengu zilizochemshwa hutoa gram 39.86 ya wanga pamoja na 17.86 g ya protini na 15.6 g ya nyuzi. Dengu pia ina madini ina fosforasi nyingi, potasiamu, kalsiamu na folate.
Vyakula vyenye wanga nyingi kupunguza au kuepuka
Watu wanaotaka kufuata lishe bora wanapaswa kuepuka soda na chipsi za viazi.
Ili kupata lishe bora, watu wanapaswa kupunguza au kuepuka wanga iliyokobolewa. Vyakula vyenye wanga nyingi ambavyo watu wanapaswa kujaribu kuepuka ni pamoja na:
● peremende
● tambi
● vitafunwa vya kukaangwa kama donati, maandazi, vitumbua na chapati
● mkate mweupe
● wali mweupe
● biskuti, muffins na bidhaa nyinginezo zilizookwa
● mtindi uliongezwa sukari
● chips za viazi
● juisi za sukari
● soda
● vyakula na vinywaji vilivyo na maji mengi ya mahindi ya fructose
● vyakula na vinywaji vilivyo na sukari iliyosafishwa kwa wingi
● vyakula vya kusindika
Mtazamo
Linapokuja suala la wanga, kanuni kuu ni kuchagua vyakula vizima na kuepuka kabohaidreti zilizosindikwa na kusagwa.
Vyakula vizima ambavyo vina wanga nyingi kwa ujumla hutoa virutubishi vingi muhimu na faida za kiafya kwa mwili. Watu walio na suala mahususi la kiafya au wasiwasi wanapaswa kuzungumza na daktari wao au mtaalamu wa lishe aliyesajiliwa ili kubaini ni vyakula gani vyenye wanga nyingi vinawafaa
.
Asante endelea kufuatilia kurasa zetu na subscribe Channel Yetu Ya Youtube tiztu kwa habari na video zote zinazohusu Afya ,chakula na mazoezi.
