Ukiwa kama mtembezi wa usiku unakua unajihatarisha kukutana na vibaka (siyo majambazi) lakini kuishi kwangu maeneo mbali mbali sijawahi kukabwa ingawa ni mtembezi mzuri tu wa usiku, ili kupunguza asilimia za kukabwa kuna mbinu zinaweza kukusaidia.

La muhimu ni kujitahidi kupunguza kumvutia kibaka akukabe, mvuto wa kukaba unaupunguza kwa kufanya haya.
1. Jinsi Unavyotembea
Mwendo wa kutompa mori kibaka akukabe ni ule wa kujiamini hatua ziwe ndefu lakini zisiwe za kuonesha kua una hamu ya kulipita eneo hilo kwa haraka. Usijitanue lakini onesha kua show ikianza hapa mtashindwa nyinyi.
Hua natembea nikiwa nimenyooka, macho yanatazama mbele na kuacha mikono iyumbe ila kiukakamavu.
2. Mavazi na Accesories zake
Usivae mavazi kama unaenda kufanya shooting halafu ni usiku, unatafutia watu dhambi. Wala nguo isiwe na nembo ambayo inaonekana dhahiri, hata viatu visiwe vya kutamanisha. Kama ni simu epuka kuitumia ikiwa na mwanga mkali au usiitumie kabisa.
Nashauri vaa pensi na shati/ vest haswa hizi vest za siku hizi zinakua kubwa kushinda mwili wa mhusika.
3. Kama unavuta sigara au bangi, tembea huku ukivuta. Kama hauvuti nunua kimoja wapo ukiwa unatembea onekana kama unavuta, ila unaweza kukutana na sungusungu ukiwa na bangi hivyo jipange kwa majibu pia.
4. Jinsi unavyoongea. Kama ukiongea una lafudhi zinazoonekana ni za kinyonge huku sauti yako ikiwa haina uzito wowote nashauri usitembee kabisa usiku.
Mfano hayo yote yamefanyika na bado vibaka wakakufuata?
Naassume haumiliki bunduki, pia naassume hauna mazoezi ya ngumi, nashauri onesha kua hautaki ugomvi na unataka suluhu hivyo ukisalimiwa itika, ukisimamishwa simama, jibu utakachoulizwa.

Jua kwamba dakika 1 kwenye ugomvi ni nyingi sana zikizidi na huna mazoezi pumzi itakuishia utaaibika, Ikiwa ugomvi utaanza tumia sekunde 30 za kwanza vizuri kwa kurusha ngumi jichoni, kutumia mawe, kutumia kichwa (kichwa piga kuanzia usawa wa pua kuja chini mdomoni), au teke la korodani.
Sekunde 30 zinazofuata ni za wewe kutoka mbio, mbio kama vile maisha yako yameshikiliwa na hizo mbio (ndiyo maana nikasema vaa pensi na vesti).
Mwisho wa yote epuka kuzurura na mwanamke usiku, hua wanatia uzito sana, na pia ni aibu kukimbia mbele ya mwanamke.
Aina za Push-Ups—na Jinsi Zinavyokusaidia
Kwanini Usimnyamazishe Mtu Akilia, Na Nini Faida Ya Kulia?
Lishe Bora Na Diet Ni nini?
Aina za Protini za poda za Kujenga Misuli
Kalori Tupu
Athari za matumizi ya pombe kiafya
Kwa nini Wanaume Hupunguza Uzito haraka?
Je,Usingizi Ni Muhimu Kiasi Gani Kwa Afya na Tunahitaji Kwa Kiasi Gani?
Aina Za Vyakula Vinavyo Ongeza Uzito Haraka
Je, Ni Nini Husababisha Uzito Kubadilika Mara Kwa Mara?
Jinsi Ya Kufanya Zoezi La (Wheel pose) Na Umuhimu Wake.
Makosa 8 yanayo fanywa zaidi na mtu anae anza mazoezi ya GYM
Je? Gramu ngapi za Mafuta – Unapaswa Kula Kwa Siku?
Fahamu mbinu za kukwepa vibaka
Je! Unapaswa Kula Kalori Ngapi Kwa Siku Ili Kupunguza Uzito?
Jinsi Ya Kufanya Mazoezi Ya Body Balance
Aina (4) Za Mazoezi Ya Kuzuia Maumivu Ya Hedhi
Jinsi Ya Kufanya Zoezi La Squat
Jinsi Ya Kutumia Tairi Katika Kujenga Mwili Wako
Vyakula Bora Kwa Kutibu Shinikizo La Damu
