Maumivu ya hedhi ni tatizo kubwa kwa wanawake wengi, hivyo zipo aina kuu za mazoezi yatakayo kusaidia kuondoa maumivu ya hedhi ukiyafanya.
1.Kutembea
Kutembea ni njia salama na nzuri inayosaidia kuujenga na kuuimarisha moyo uwe na afya nzuri na usio katika hatari ya kushambuliwa na maradhi. Mazoezi au tabia ya kufanya mazoezi inayo faida kubwa zaidi kuliko matumizi ya dawa.
1. Mazoezi husaidia kupunguza uzito, tembea lisaa limoja kila siku 2. Ni mazoezi yanayoweza kufanywa na kila mtu 3. Ni mazoezi yasiyohitaji vifaa/hayana gharama 4. Ndiyo njia rahisi kabisa ya kuufanya mwili kuwa mkakamavu 5. Hupunguza dalili za majonzi na wasiwasi 6. Ni mazoezi yenye matokeo ya taratibu 7. Hupunguza uwezekano wa kupatwa na kolesto/lehemu 8. Hupunguza na kutibu shinikizo la damu 9. Hupunguza uwezekano wa kupatwa na baadhi za kansa 10. Hupunguza uwezekano wa kupatwa na kisukari 11. Hukufanya ujisikie vizuri 12. Husaidia kuimarisha mifupa 13. Husaidia kupunguza uwezekano wa kupatwa na shambulio la moyo 14. Ni mazoezi uwezayo kuyafanya bila kukusababishia ajari au maumivu makubwa 15. Hupunguza mfadhaiko/stress 16. Hupunguza uwezekano wa kupatwa na ugonjwa wa moyo 17. Ni mazoezi unayoweza kuyafanya bure bila kulipia chochote 18. Husaidia kuimarisha mishipa 19. Husaidia katika mfumo wa upumuwaji 20. Husaidia kuongeza mzunguko wa damu
unaweza kua unatembea ukiwa ndani ya nyumba yako au umbali flani mdogo nk
02 kucheza
Imejulikana kwa miaka mingi kuwa mazoezi ya mwili na mazoezi ya michezo hutoa faida nyingi za mwili, kwa mfano kusaidia kuboresha utendaji wa mifumo ya upumuaji, mzunguko wa damu na mifupa. Lakini tunapocheza, tunapata faida za mazoezi ya mwili ya aerobic, na pia tunafaidika kwa kiwango cha kisaikolojia na kihemko
mwanamke au msichana anapokua kwenye hedhi maranyingi anakua na mawazo na stress nyingi sana,hivyo kuuburudisha mwili kwa kucheza mziki unapunguza stress na mawazo uliyo kua nayo
03 yoga
mazoezi ya yoga husaidia kutuliza akili
kunyoosha misuli
kuunganisha mwili pamoja na akili zako
husaidia kuondoa msongo wa mawazo
04 mazoezi ya balance
mazoezi ya balance yanahusisha zaidi sehem yakati ya mwili wako ambapo nguvu ya kani ilipo pia ni sehemu ambapo viungo vya uzazi vilipo hivyo unapo fanya mazoezi ya balance yanakusaidia kuondoa maumivu
1.kufanya mzunguko wako wa hedhi uwe vizuri
2..kuondoa stress
3.kuondoa maumivu
4.Hufanya uwe na furaha ukiwa katika siku zako
05.Mazoezi ya kujinyoosha(stretching)
mara nyingi maumivu wakati wa hedhi hutokea kwasababu viungo vinakua vimebana ile damu chafu wakati inatoka misuli ya ndani inakua inavuta na kuachia.
kwahiyo utakapo kua unafanya mazoezi ya kujinyoosha unasaidia ile misuli iweze kulegea na kukaa vizuri hivyo kupunguza maumivu wakati wa hedhi
07 mazoezi ya kutafakali(meditation)
Hii ni kama kusali, kaa sehemu tulivu
kusikiliza nyimbo nzuri za kutafakalisha mazoezi haya yanasaidia kujipa mtumaini
hivyo kupunguza mawazo na kufanya mwili wako kujirudi katika hali ya kawaida
Kitu cha kuzingatia ni kua usizidishe sana mazoezi haya, kwani kutafakali sana kunaweza kuongeza zaidi mawazo akilini mwako. Pia kama wewe ni mtu wa mazoezi jaribu kuchanganya na mazoezi mengine kama vile kukimbia, kutembeana na aina nyingine yeyote ya mazoezi madogo madogo.
Zingatia unapo kua kwenye siku zako hauhitaji kufanya mazoezi magumu
Asante endelea kufuatilia kurasa zetu na subscribe Channel Yetu Ya Youtube tiztu kwa habari na video zote zinazohusu Afya ,chakula na mazoezi.
https://youtu.be/RcxdLwC-reg Kalori ni nini? Kwa ufupi, kalori ni kitengo kinachopima nishati. Kalori hutumiwa kupima maudhui ya nishati ya vyakula na...
https://www.youtube.com/watch?v=iE8k-i0X9Xk&t=1s Jinsi Ya Kufanya Mazoezi Ya Body Balance Mazoezi ya Body balance yanasaidia sana katika msawaziko wa mwili na katika...
https://www.youtube.com/watch?v=qQiuay9fzAQ&t=1s Aina (4) Za Mazoezi Ya Kuzuia Maumivu Ya Hedhi Maumivu ya hedhi ni tatizo kubwa kwa wanawake wengi, hivyo...
https://www.youtube.com/watch?v=66VqjncGw0o Jinsi Ya Kufanya Zoezi La Squat Japo kuwa Squat ni zoezi zuri sana, lakini ukilikosea linaweza kukupa madhara badala...
https://www.youtube.com/watch?v=BoHY7B4M_EE Jinsi Ya Kutumia Tairi Katika Kujenga Mwili Wako Tairi ni moja ya nyenzo muhimu sana itakayo kusaidia katika mazoezi...
https://www.youtube.com/watch?v=QDu-HMqozgA&t=1s Kubadilisha lishe kunaweza kupunguza kwa kiasi kikubwa shinikizo la damu. Utafiti umeonyesha kuwa vyakula fulani vinaweza kupunguza shinikizo la...